Nawaomba muangalie hii habari kuhusu matatizo ambayo tunayo na yatakayo tukumba.
Mwisho, tuweze kutunza mazingira yetu na kuweza kuelimisha jamii nzima kuhusu mazingira na tuweze kutumia maji tuliyo nayo kwa uangalifu.
Siku zote majibu ya maswali mengi yanapatikana tukiwa tukijiuliza, je hivi ni kwanini inakuwa hivi? au je kwanini isiwe hivi? Basi pale utakapo anza kujiuliza haya maswali mara nyingi utapata majibu!
Jinsi nilivyo anza na hayo maneno hapo juu ni kwamba nataka kuzungumzia kuhusu swala ambalo nataka tuweze kunufaika sote wana-blog ambapo Mara nyingi ukiangalia blog zetu utakuta kuna msululu wa archives, msululu wa previous posts (Last posts) basi inaleta karaha kubwa (Picha Mbaya) kutokana na hiyo misululu na hii inaendana na kama mtu ukiwa una posts nyingi za zamani!
Pia tukiangalia blog zetu ktk Archives siku zote posts zile mpya zinakuwa chini na za zamani zinakuwa juu sasa baada ya kuweka code mpya za leo zitakufanya blog yako iwe na uwezo wa kuonesha ktk Archives Post mpya kwanza na kufuatia na post za zamani!!
Sasa jawabu la hilo swali au tatizo mwisho wake ni leo 25th April 2006 11:19:30am GMT+1 ambapo nakuja na code ambazo zitaondoa kabisa hiyo misululu isiyo kuwa na mwisho!
Yafuatayo ni maelekezo ya kufanya:
1: Sign In ktk Blog yako.
2: Ukifika ktk Dashboard, Click Change Settings alafu tena click Template.
3: Ukiwa ndani ya Template tafuta wapi yalipo haya maandishi,haya ni maandishi yaliyopo ktk template yangu sasa nina uhakika asilimia 99.99 ya kwamba ktk blog zenu kutakuwa na kitu kama hiko hiko. kwa kifupi, haya maandishi yapo mwisho mwisho wa code za blog zenu sasa mkifika ktk template nenda chini (mwisho wa code) na uanze kuangalia wapi hayo maandishi yalipo.
4: Baada ya kuyapata, Badilisha (Futa) maandishi yoyote yanayo endana na Archives au Previous Post (Last Posts) na nawaomba muweke hizi code.
Hizi code ni za Archives pamoja na Previous Posts (Last Posts) sasa ukiwa unafuta code kumbuka kuweka code zitakazo kwenda kuziba pengo lililowachwa wazi pia kuwa muangalifu usije kufuta code zisizo endana na Archives au Previous Post (Last Posts).
Kama kukiwa na tatizo au maswali yoyote nitafurahi kuweza kuyajibu au kutoa ushauri wowote, cha kufanya ni kuniandika hapa ktk hii blog au nitumie e-mail na nitakujibu asap.
Nashukuru.
Baada ya kukaa chini muda mrefu na kuweza kugundua code zinazo ondoa Blogger NavBar (Ile Search Box iliyopo juu ya blog yako) hii ni kutokana watu wengi hawaipendi Blogger NavBar. lakini kutokana ya kwamba hakuna njia nyingine ya mtu ku-search kwa urahisi nakala ulizo andika nyuma (zilizopita) ilibidi watu wengi waache Blogger NavBar kama ilivyo!!
Sasa nimerudi tena na kuweza kugundua code mpya zitakazo wezesha mimi na wewe kuondoa Blogger NavBar na vile vile kuendelea kuwa na uwezo wa ku-search nakala zako zilizo pita.
Yafuatayo ni maelekezo ya kufanya hivyo:
A: Fanya yale maelekezo niliyo andika mwanzo ili uweze kuondoa Blogger NavBar naomba usome kupitia hapa. , Baada ya kuweza kuondoa Blogger NavBar fuata haya maelekezo:
B: Copy code zifuatazo (Chagua moja wapo la kundi yafuatayo hapa chini kutokana na mapendekezo yako) na nenda ktk Sign in ktk Blog yako-->Dashboard-->Change Settings-->template na uweze kuchagua ni mahali gani unataka hii Search Box yako iweze kutokea. Baada ya kuchagua na kupata sehemu ya kuweka code zako (sehemu ya kutokea search box yako) Paste code ulizo zi-copy. Kama unataka kuona search box yako imekaa sehemu unayo itaka (unayo ipenda) click Preview kabla ya ku-click Save Template Changes au ku-Click Republish your Blog. Endelea kufanya hivyo mpaka utakapo pata sehemu unayo ipenda.
C: Katika hizi code utakuta neno YOUR DOMAIN NAME futa hayo maandishi na weka anuani ya website yako yaani mfano: value="YOUR DOMAIN NAME" name.. na iwe hivi: value="http://vijimamboz.blogspot.com" name hivyo ndio mfano kama ingekuwa ni mimi naweka hizo code sasa badilisha kutokana na anuani yako ya blog. Fanya hivyo popote pale utakapo ona hilo neno ktk code zifuatazo hapa chini.
D: Click Save Template Changes alafu Click Republish your Blog.
Kutokana ni vigumu kuweza kuweka hizo code hapa maana zinakataa kuji-publish na kutokea kama page, nawaomba msome kupitia hapa. (Right click na chagua open in new window) ili ifunguke ktk page nyingine.
utaitaji ms-word kufungua hili file.
Kumbuka watu wengi hawaipedi Navbar kutokana inazuia kuweza kuweka vitu vingi ktk site yako mfano: calendar, saa na vitu vingi ambavyo vinaitaji viwepo juu ya site yako, Vile vile inaleta picha mbaya.
Kama una maswali au Tatizo zaidi kuhusu hili swala naomba niandikie na nitakujibu asap.
Nashukuru.