Thursday, June 15, 2006

UPUNGUFU WA MAJI ULIMWENGUNI NI CHANZO CHA VITA YA BAADAE.
Uhalibifu wa mazingira na vyanzo vya maji pamoja na harakati za kibinadamu ktk kujitafutia maendeleo kutokana na majaribia mbali mbali yanayo haribu mazingira ni vyanzo vikuu vikubwa vinavyo sababisha upungufu wa maji ulimwenguni.

Kama ilivyo kwa thamani ya bidhaa za madini mbali mbali, Petrol, Diesel pamoja mafuta ya taa ambayo inayo fanya au kuleta vita hapa duniani ndivyo itakavyo kuwa ktk hii bidhaa muhimu (maji) ktk maisha ya binadamu ambayo ina muwezesha kuweza kuishi na hapo ndipo binadamu tutaweza kupigana vita kwa sababu ya upungufu wa maji.


Kama binadamu wa sasa hawezi kutunza mazingira yake pamoja na vyanzo vya maji basi matatizo makubwa yanaweza kutukumba, Baadhi ya hayo matatizo tunayaona sasa ambapo kila kona ya ulimwengu kuna upungufu wa maji. i.e Kama tunavyo fahamu uchumi wa nchi nyingi ulimwenguni unategemea kilimo ambapo hiko kilimo kinategemea maji sasa kama hakuna maji basi uchumi wa mataifa mengi utakuwa mbaya ambapo utazoretesha uduma mbali mbali za kijamii, n.k

Nawaomba muangalie hii habari kuhusu matatizo ambayo tunayo na yatakayo tukumba.

Mwisho, tuweze kutunza mazingira yetu na kuweza kuelimisha jamii nzima kuhusu mazingira na tuweze kutumia maji tuliyo nayo kwa uangalifu.