Thursday, May 18, 2006


HISTORIA YA AIRBUS A380 NDANI YA UK
Ndege ya abiria aina ya Airbus A380 yenye viti vya abiria 555 ambayo ni kubwa kuliko zote ulimwenguni imeweza kuingia ktk historia ya kuwa ni ndege ya kwanza ya aina hiyo kutua ktk ardhi ya Uingereza ktk uwanja wa ndege wa Heathrow hii leo 18/05/2006 saa 13:20 mida ya Uingereza ikitokea Berlin, Germany.

Maandalizi ya kuwezesha ndege hiyo kutua ktk uwanja wa Heathrow imewagarimu waingereza ( British Airports Authority) jumla ya 450 Million pounds na pia imetua ktk sehemu impya ( Inayo julikana kama pier 6 ktkTerminal 3) iliyo jengwa na kugarimu jumla ya 105 Million pounds.

Airbus A380 itakuwa ni mshindani mkubwa wa ndege za Boeing, na kuonesha Boeing wapo ktk ushindani nao wametengeneza ndege aina ya 787 Dreamliner kuweza kushindana ambayo inategemewa kuingia ktk soko ifikapo mwaka 2008 na kuweza kubeba abiria kati ya 200 mpaka 350.

Jumla ya gharama zilizo wezesha kutengeneza ndege ya Airbus A380 ni 6 Billion pounds ambapo mpaka sasa kampuni ya Airbus S.A.S imepokea order karibia 159 kutoka kwa mashirika 16 ya ndege zinazotaka kununua aina hii ya ndege.

Bonyeza hapa kusoma orodha ya makampuni na idadi ya ndege walizo order.

Bonyeza hapa kuona video mbali mbali za Airbus A380 pia kama ukitaka kuangalia video nyinginezo zinapatikana kwa kubonyeza hapa.

Mwisho, ingawa hii ni kama historia lakini imeleta mitazamo tofauti ambapo kuna makundi mawili, yanayo kubaliana na technology hii na wanao ipinga kutokana na sababu za mazingira.

Tuesday, May 16, 2006

Kama ukitaka blog yako ipendeze zaidi, basi unaweza kuweka hizi code ili kuweza kufanya scrollbar yako kubadilika rangi au iwe na rangi tofauti tofauti. Unaweza kuangalia scrollbar ktk blog yangu na kuona ninacho sema.

Unaweza kubadili rangi tofauti tofauti kutokana na mapendekezo yako, na utaweza kufanya hivyo ktk sehemu zenye maandishi kama #FFFFFF; #6DA4FF; #ACA899; black; #FFFFFF; na kufuta #FFFFFF, #6DA4FF, #ACA899, black au #FFFFFF na kuandika rangi unayotaka eidha kwa kutumia code kama nilivyo andika mwanzo au kwa maandishi mfano pink, green, red, n.k.

Kumbuka ukiandika kwa code au kwa maandishi andika kwa usahii na kwa kiingereza tu na msifute alama hii ; yaani ukiandika red iwe red; au #ff0000; hivyo ndivyo ingekuwa kwa kutumia code nikiwa nina maanisha rangi nyekundu.

Yafuatayo ndio maelekezo ya kufanya:

1: Sign In ktk Blog yako

2: Ukifika ktk Dashboard,Click->Change Settings->Template

3: Ukifika ktk template, tafuta wapi yalipo haya maandishi head yakianza na tag < na kuishia na tag > na baada ya kuyapata hayo maandishi chini yake weka code zifuatazo.

4: Mwisho, click save template changes alafu click republish your blog.

Na hapo utakuwa umemamaliza kila kitu.

Tuesday, May 09, 2006

NA NYINGINE HIYO!!
Leo nawaletea code nyingine kwa wale wenye blog ndefu au blog za picha ambazo ni ndefu.

Code hizi ni kuwawezesha wasomaji wenu kuweza kupelekwa juu (Mwanzo) pale wafikapo mwisho bila ya kuangaika kwenda juu. Mfano wake upo ukiangalia chini ya hii blog (Vijimamboz) utaona kuna kijisehemu kina kwambia rudi juu na uki-click hapo unakwenda juu.

Maelekezo ni kama kawaida, Ambayo ni:
1(a): Sign In ktk Blog yako

1(b): Ktk Dashboard,Click->Change Settings->Template

1(c): Ukifika ktk template, Chagua ni wapi unataka hiyo button iweze kukaa (Ni vizuri ukiweka chini kabisa maana wasomaji wenu wakishafika mwisho wa blog tu waweze kukibonyeza na kupelekwa juu) na alafu muweke hizi code.

1 (d): Mwisho, click save template changes alafu click republish your blog.

Na hapo utakuwa umemamaliza kila kitu.

Sunday, May 07, 2006

JE UNAMJUA GARY MCKINNON?
Gary Mckinnon kwa jina lingine anajulikana kama Solo (Miaka 39) ni hacker raia wa Uingereza ambaye ktk historia za ma-hacker anajulikana kama ni mtu pekee aliyeweza ku- hack computer 97 muhimu sana za jeshi la Marekani na computer za NASA kati ya mwaka 2001 - 2002, Nikizungumza Jeshi la Marekani nina maanisha majeshi yote ya Marekani.

Gary Mckinnon aliweza kukamatwa mwaka 2002 baada ya kugunduliwa na kikosi cha uingereza kijulikanacho kama National Hi-Tech Crime Unit (NHTCU) na alikamatwa kutokana na sheria ijulikanayo kama Computer Misuse Act.

Hivi sasa bwana Gary Mckinnon yupo nje kwa masharti ya kwamba kila siku jioni ni lazima aweze ku-report ktk kituo cha polisi, Haruhusiwi kutumia Computer yoyote ile yenye huduma ya Internet, na ni lazima kila siku alale nyumbani kwao.

Mpaka sasa kesi inaendelea nchini Uingereza na Serikali ya Marekani imeiomba Serikali ya Uingereza impeleke bwana Gary Mckinnon nchini Marekani waweze kumshitakia ndani ya Marekani, Kama akipelekwa Marekani na kupatikana na hatia anakabiliwa kufungwa si chini ya miaka 70 ndani ya jela.

Kama unataka kuangalia video yake ikimuonesha akielezea jinsi alivyo fanya hayo mambo naomba bonyeza hapa.

Mwisho, Ndugu wasomaji nawaomba muwe makini na watu kama hawa na siku zote akikisha computer zenu zina ulinzi wa kutosha sababu kama mtu huyu ana uwezo wa ku-hack computer za Serikali ya Marekani basi watu kama hawa wana uwezo wa ku-hack computer zetu, za Serikali yetu na mashirika yote ndani ya Tanzania.

Kwa habari zaidi endelea kutembelea Vijimamboz

Saturday, May 06, 2006


NI NANI WA KUOKOA DARFUR NA AFRIKA?

Hapa uliwenguni ni mahali pazuri na pabaya kuishi, Ni pazuri kama tukiwa na Amani na Upendo na Vile vile kunakuwa ni pa chungu kama Amani na Upendo ukitoweka.

Dhumuni la nakala hii ni kuonesha au kuuliza ni nani atakae okoa Wananchi Darfur na Afrika kwa ujumla hasa hasa watoto na akina Mama? Kwa Mfano hapo Darfur ni tatizo la siku nyingi likiwa linaendelea kila siku na Viongozi wetu wa hii dunia wakibaki kuliangalia tu kama vile hawalioni!! Wanabaki wakiliangalia na kuacha ma-million ya wananchi wakiteseka na kufa kwa njaa au kuuana wenyewe kwa wenyewe.

Vile vile hata Serikali yenyewe ya Sudan inabaki midomo imefunga na kuliangalia hilo swala ata pia wakiweza kudhamini ata wale magaidi (The Janjaweed) wanao ua kila siku watoto, wanawake, na wanaume!!

Nchi nyingi za Afrika wanajifanya kama hawalioni hili swala na kuna wakati walijifanya wanaona na kupeleka majeshi ya AU (Askari 7,000 tu) lakini cha kushangaza hayo majeshi hayafanyi chochote kuzuia Vifo vya watoto, wanawake, na wanaume.

Dunia inajifanya inaona na kutaka kusaidia lakini inapofika kusema kuiwekea Serikali ya Sudan Vikwazo na kupeleka majeshi ya UNO kulinda Amani, Utaona baadhi ya nchi zinazopata maslahi toka Sudan zikizua hilo pendekezo hii ikijumuisha nchi ya China ambayo imewekeza zaidi ya 3 Billion US Dollars ktk Mafuta ya Sudan na hizo hizo pesa ndizo zinazo dhamini Silaha zinazo leta hivi Vifo.

China imekuwa nchi ambayo haifuati haki za binadamu na Sheria ambapo kutokana siku hizi imekuwa Super Power ktk hii dunia basi matumizi yake pia yanakua ambayo yanafanya kutafuta soko la mahitaji yake bila hata ya kufuata sheria (Kufumba Macho mabaya yafanywayo na Serikali zinazo mpatia hayo mahitaji) hii ikijumuisha Kenya- Haikemei Rushwa inayo endelea, n.k, Zimbabwe- Haikemei uvunjwaji wa haki za binadamu, n.k, Sudan- Haikemei Uvunjwaji wa haki za binadamu, na pia ndio inazuia muswada usipitishwe ktk Umoja wa mataifa kwakuwa ina kura ya Veto, Chad- Haikemei uvunjwaji wa haki za binadamu na watu wanakufa na njaa huku kiongozi wa nchi hii akiishi maisha ya kifalme na kununua magari ya kifahari!! Hii mifano sio kwa nchi za Afrika tu bali ktk nchi nyingi hapa duniani, Yaani nina mifano mingi tu hii ikijumuisha mataifa mengi hacha China tu.

Mpaka nina andika hii nakala baadhi ya vikundi ndani ya Sudan havikuweza kuweka sahii ktk makubaliano ya Amani!!

Kwa Ufupi tu hapa nina uliza ni nani atakae kuja kutukomboa ktk haya matatizo tuliyo nayo Afrika?

Ni nani atakae kuja kuokoa watoto, Wakina Mama, Wakina Baba wa Darfur?

Kwanini wanaendelea kuuza Silaha kwa nchi za Afrika zenye machafuko zinazo fanya kuuana wenyewe kwa wenyewe?

Wako wapi Viongozi wa Afrika na hii dunia?

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibarika Afrika.

Nashukuru.

Wednesday, May 03, 2006

MAMBO MAPYA
Je ulishawahi kuwa na website au Blog na baadae ukaamua kutengeneza website au blog nyingine kutokana na sababu mbali mbali?

Kama jibu ni ndio ni wazi kwamba baadae uliweza kuwataharifu ndugu, jamaa na marafiki kama umebadilisha anuani ya website au blog ile ya zamani na kuamua kuwapa anuani mpya ili waweze kukutembelea ktk makazi mapya.

Sasa leo hii nakuja na code zitakazo kukuondolea tatizo la kuambia watu wote kwamba anuani yako ya website imebadilika, cha kufanya hapa ni kufuata malelekezo yafuatayo:
1(a): Sign In ktk Blog ile ya zamani

1(b): Ukifika ktk Dashboard, Click -->Change Settings-->Template

1(c): Ukifika ktk Template tafuta wapi yalipo haya maandishi head yakianza na tags < na kuishia na tag > na baada ya kuyapata hayo maandishi chini yake weka code zifuatazo, bonyeza hapa kuzipata.

2 (a) Utafanya hivyo hivyo ata ktk website yako ambayo ni tofauti na blog, Chakufanya nenda ktk sehemu zilipo code zinazo tengeneza website yako na tafuta maandishi head yakianza na tag < na kuishia na tag > ambayo yapo mwanzo mwanzo mwa code zilipo anzwa kuandikwa na uweke hizi code.

Kuna code za aina mbili ambazo kazi zake zote ni za aina moja sasa mtachagua ni code zipi mtazitumia ktk ya hizo mbili (Yaani chagua moja tu).
Ukikuta sehemu nimeandika "weka anuani mpya hapa" unabidi muweke anuani zenu za website au blog mpya mfano http://vijimamboz.blogspot.com hii ni kama ingekuwa mimi.

3: Mwisho, click save template changes alafu click republish your blog au wenye website tofauti na blog click Save changes.

Basi baada ya kumaliza hapo tu watu wakiwa wanaenda ktk ile website au blog ya zamani watapelekwa moja kwa moja katika makazi mapya ( Yaani ktk website au blog yako mpya).

Ukiwa na maswali zaidi kuhusu hii nakala naomba niandikie na nitakujibu asap.

Nashukuru.