Tuesday, April 25, 2006

SAA YA KUONDOA MSULULU NDANI YA BLOG NI SASA.

Siku zote majibu ya maswali mengi yanapatikana tukiwa tukijiuliza, je hivi ni kwanini inakuwa hivi? au je kwanini isiwe hivi? Basi pale utakapo anza kujiuliza haya maswali mara nyingi utapata majibu!

Jinsi nilivyo anza na hayo maneno hapo juu ni kwamba nataka kuzungumzia kuhusu swala ambalo nataka tuweze kunufaika sote wana-blog ambapo Mara nyingi ukiangalia blog zetu utakuta kuna msululu wa archives, msululu wa previous posts (Last posts) basi inaleta karaha kubwa (Picha Mbaya) kutokana na hiyo misululu na hii inaendana na kama mtu ukiwa una posts nyingi za zamani!

Pia tukiangalia blog zetu ktk Archives siku zote posts zile mpya zinakuwa chini na za zamani zinakuwa juu sasa baada ya kuweka code mpya za leo zitakufanya blog yako iwe na uwezo wa kuonesha ktk Archives Post mpya kwanza na kufuatia na post za zamani!!

Sasa jawabu la hilo swali au tatizo mwisho wake ni leo 25th April 2006 11:19:30am GMT+1 ambapo nakuja na code ambazo zitaondoa kabisa hiyo misululu isiyo kuwa na mwisho!

Yafuatayo ni maelekezo ya kufanya:

1: Sign In ktk Blog yako.

2: Ukifika ktk Dashboard, Click Change Settings alafu tena click Template.

3: Ukiwa ndani ya Template tafuta wapi yalipo haya maandishi,haya ni maandishi yaliyopo ktk template yangu sasa nina uhakika asilimia 99.99 ya kwamba ktk blog zenu kutakuwa na kitu kama hiko hiko. kwa kifupi, haya maandishi yapo mwisho mwisho wa code za blog zenu sasa mkifika ktk template nenda chini (mwisho wa code) na uanze kuangalia wapi hayo maandishi yalipo.

4: Baada ya kuyapata, Badilisha (Futa) maandishi yoyote yanayo endana na Archives au Previous Post (Last Posts) na nawaomba muweke hizi code.
Hizi code ni za Archives pamoja na Previous Posts (Last Posts) sasa ukiwa unafuta code kumbuka kuweka code zitakazo kwenda kuziba pengo lililowachwa wazi pia kuwa muangalifu usije kufuta code zisizo endana na Archives au Previous Post (Last Posts).

Kama kukiwa na tatizo au maswali yoyote nitafurahi kuweza kuyajibu au kutoa ushauri wowote, cha kufanya ni kuniandika hapa ktk hii blog au nitumie e-mail na nitakujibu asap.

Nashukuru.


Wednesday, April 12, 2006

Je unafahamu hii?
Je ulidhani ya kwamba mtu kutokuwa na password yako au jina unalotumia hawezi kujua code zilizo tengeneza blog au website yako? Kama ulikuwa una waza hivyo naomba usiwaze tena maana kuna njia moja wapo ambayo mimi ninafikiri njia hii ni kutokamilika kwa internet (Ubaya wa internet).

Sasa ebu tuangalie ni jinsi gani utakavyo gundua code za mtu mwingine zilizotengeneza blog yake! Kwanza kabisa naomba u-right click mouse yako alafu tafuta maandishi yaliyoandikwa View Source baada ya kuyapata jaribu ku-click (Ingia) ktk hayo maandishi basi baada ya hapo utajua code zilizotengeneza hiyo website au blog pia utajua mambo mengi zaidi ukiziona hizo code.

Sasa basi kutokana ya kwamba internet ni chombo kizuri na kibaya pia nimeweza kuwaletea dawa itakayo ondoa hilo tatizo. Dawa yenyewe itaenda kutibu pale palipo na tatizo ambapo ni kuweza kuzima uwezo wa mtu yoyote kuweza ku-right click akiwa ndani ya blog au website yako!!

Yafuatayo ni maelekezo ya kuweza kuzima right click mouse:

1: Sign In ktk Blog yako

2: Ukifika ktk Dashboard, Click "Change Settings" alafu Click sehemu ya "Template".

3: Ukishafika kwenye Template tafuta wapi yalipo haya maandishi: <body>

4: Baada ya kuyapata hayo maandishi chini yake weka haya maandishi:

Kutokana na ya kwamba blog inakataa kuonesha hizi code naomba bonyeza hapa kuweza kuzipata hizi code.

5: Baada ya kuzipata hizo code fanya kama nilivyo elekeza hapo juu (3 - 4) alafu mwisho wake naomba click save template changes alafu click republish your blog.
Kuanzia sasa utakuwa umeweza kuzuia watu wasione viungo vinavyotengeneza blog au website yako!!!

Kuanzia leo ukitaka ku-copy kitu chochote kwanza chagua cha kuweza ku-copy (select, highlight) alafu unabonyeza ctrl+c au ukitaka ku-paste kitu chochote utabonyeza ctrl+v. Ninapo andika ctrl+v au ctrl+c nina maanisha kwanza bonyeza ctrl ukifuatia na v au c kwa wakati mmoja yaaani usiachie kile ulicho bonyeza mwanzo ukiwa unabonyeza cha pili. Naomba angalia keyboard yako.

mwisho, kumbuka hii inazuia website au blog yako tu hivyo basi utakuwa na uwezo wa ku-right click ktk website nyingine au blog nyingine.

Ukitaka kuweza kuweka ulinzi mzuri ktk computer yako kumbuka kununua software zitakazo linda computer yako, unaweza ku-download vitu vifuatavyo ambavyo ni bure (Download zote mbili):

1: Malicious Software Removal Tool

2: Windows Defender (Beta 2)

3: Kwa ulinzi zaidi baada ya ku-download hivyo vitu hapo juu, wale wanaotumia window xp mnaweza kuimalisha ulinzi kwa kubonyeza Start --> Control Panel --> Security Center--> Na uweze kuona kama Firewall ipo ON, Microsoft Automatic updates ipo ON, Virus Protection ipo ON. Kama hivyo vitu vipo OFF unaweza kuviweka ON na ktk Firewall weka ON alafu chagua don't allow exceptions na mwisho click OK. Kwa ujumla ukifika ktk Security Center utapata maelezo zaidi ya kufanya. Pia kama unatumia window xp service pack1 nakushauri nenda microsoft. na uweza ku-download window xp service pack2 kwasababu sp2 ni imara zaidi kwa ulinzi wa computer yako kuliko sp1.

Software nyingine ambazo ni bure zitakazo weza kulinda computer yako ni (Chagua moja kati ya hizi):

A: Lavasoft Ad-Aware SE

B: Spybot Search & Destroy (S&D)

Kama una pesa ya kununua software mimi naunga mkono (napendekeza) hii bonyeza hapa kusoma zaidi maana hii ni imara sana.

Kumbuka ya kwamba kama ukiwa na software moja usichanganye na nyingine maana zitakuwa zinaingiliana kulinda computer yako na kuweza kufanya hackers kuiba siri zako zilizopo ktk computer yako. Pia kumbuka usi-download kitu chochote usicho kijua ata kama ni kizuri kiasi gani soma kwanza maelezo yote na ndio download au usifungue e-mail yoyote kama hamjui mtu aliye ituma.

Pia unaweza kubonyeza tools hapo juu-->Internet Options-->Security: Internet-->Medium, Local Intranet--> Medium, Trusted Sites--> Medium, Restricted Sites--> High kila unapokuwa ukibadilisha click apply.
Ukiwa hapo hapo ktk Internet Options--> Privacy: Medium High alafu chagua block popups maana popups nyingi ni mwanzo wa spyware na virus wengine. Kama ukitaka kuruhusu popups ambazo unaziamini siku zote bonyeza Ctrl na wakati huo huo click ktk sehemu husika.

Unaweza kujifunza zaidi kwa kuangalia video zifuatazo bonyeza hapa pia angalia hii video.

Kwa habari zaidi kuhusu software mbali mbali bonyeza hapa au unaweza kutembelea microsoft.

Ukiwa na maswali zaidi kuhusu hii nakala naomba niandikie na nitakujibu asap.


Nashukuru.


Wednesday, April 05, 2006

JAWABU LIMEPATIKANA:

Baada ya kukaa chini muda mrefu na kuweza kugundua code zinazo ondoa Blogger NavBar (Ile Search Box iliyopo juu ya blog yako) hii ni kutokana watu wengi hawaipendi Blogger NavBar. lakini kutokana ya kwamba hakuna njia nyingine ya mtu ku-search kwa urahisi nakala ulizo andika nyuma (zilizopita) ilibidi watu wengi waache Blogger NavBar kama ilivyo!!

Sasa nimerudi tena na kuweza kugundua code mpya zitakazo wezesha mimi na wewe kuondoa Blogger NavBar na vile vile kuendelea kuwa na uwezo wa ku-search nakala zako zilizo pita.

Yafuatayo ni maelekezo ya kufanya hivyo:

A: Fanya yale maelekezo niliyo andika mwanzo ili uweze kuondoa Blogger NavBar naomba usome kupitia hapa. , Baada ya kuweza kuondoa Blogger NavBar fuata haya maelekezo:

B: Copy code zifuatazo (Chagua moja wapo la kundi yafuatayo hapa chini kutokana na mapendekezo yako) na nenda ktk Sign in ktk Blog yako-->Dashboard-->Change Settings-->template na uweze kuchagua ni mahali gani unataka hii Search Box yako iweze kutokea. Baada ya kuchagua na kupata sehemu ya kuweka code zako (sehemu ya kutokea search box yako) Paste code ulizo zi-copy. Kama unataka kuona search box yako imekaa sehemu unayo itaka (unayo ipenda) click Preview kabla ya ku-click Save Template Changes au ku-Click Republish your Blog. Endelea kufanya hivyo mpaka utakapo pata sehemu unayo ipenda.

C: Katika hizi code utakuta neno YOUR DOMAIN NAME futa hayo maandishi na weka anuani ya website yako yaani mfano: value="YOUR DOMAIN NAME" name.. na iwe hivi: value="http://vijimamboz.blogspot.com" name hivyo ndio mfano kama ingekuwa ni mimi naweka hizo code sasa badilisha kutokana na anuani yako ya blog. Fanya hivyo popote pale utakapo ona hilo neno ktk code zifuatazo hapa chini.

D: Click Save Template Changes alafu Click Republish your Blog.

Kutokana ni vigumu kuweza kuweka hizo code hapa maana zinakataa kuji-publish na kutokea kama page, nawaomba msome kupitia hapa. (Right click na chagua open in new window) ili ifunguke ktk page nyingine.

utaitaji ms-word kufungua hili file.

Kumbuka watu wengi hawaipedi Navbar kutokana inazuia kuweza kuweka vitu vingi ktk site yako mfano: calendar, saa na vitu vingi ambavyo vinaitaji viwepo juu ya site yako, Vile vile inaleta picha mbaya.

Kama una maswali au Tatizo zaidi kuhusu hili swala naomba niandikie na nitakujibu asap.

Nashukuru.

Monday, April 03, 2006

Baada ya uchunguzi wa siku nyingi na wa hali ya juu nimegundua jawabu la kuondoa Blogger NavBar (Sehemu ya juu kabisa ya Blog yako inayo onesha search this blog). Hii kutokana na ya kwamba watu wengi uwa wanachukizwa na jinsi hiyo NavBar ilipo.

Jawabu la hili swali ni:

1: Sign in ktk Blog yako.

2: Ukifika ktk Dashboard, Click "Change Settings" alafu Click sehemu ya "Template".

3: Ukishafika kwenye Template tafuta wapi yalipo haya maandishi:
link rel="stylesheet" type="text/css" href="style.css"/>
/*

au blog zingine kuna maandishi haya:
style type="text/css"
/*

Hapa kwenye template ni sehemu inayo ifadhi code ambazo zinazotengeneza blog yako. Sasa basi mara nyingi hayo maandishi yapo mwanzo mwanzo wa code zinapoanzwa kuandikwa. Sasa usiangaike kwenda chini zaidi au katikati, Wewe Unapofika kwenye template tu angalia mwanzoni na utaona hayo maandishi.

4: Baada ya kupata hayo maandishi naomba chini yake weka haya maneno: #b-navbar{ margin-top: -500px;}

Kumbuka haya maneno ndio dawa ya kuondoa NavBar. Narudia tena dawa ni #b-navbar{ margin-top: -500px;}

Baada ya kumaliza ni lazima maandishi yaonekane kama hivi:
link rel="stylesheet" type="text/css" href="style.css"/>
#b-navbar{ margin-top: -500px;}
/*

Wenye blog zingine zionekane kama hivi:
style type="text/css"
#b-navbar{ margin-top: -500px;}
/*

5: Mwisho: Click Save Template Changes alafu Click Republish your Blog.

Kama una maswali au Tatizo zaidi niandikie.

Nashukuru.