Wednesday, April 12, 2006

Je unafahamu hii?
Je ulidhani ya kwamba mtu kutokuwa na password yako au jina unalotumia hawezi kujua code zilizo tengeneza blog au website yako? Kama ulikuwa una waza hivyo naomba usiwaze tena maana kuna njia moja wapo ambayo mimi ninafikiri njia hii ni kutokamilika kwa internet (Ubaya wa internet).

Sasa ebu tuangalie ni jinsi gani utakavyo gundua code za mtu mwingine zilizotengeneza blog yake! Kwanza kabisa naomba u-right click mouse yako alafu tafuta maandishi yaliyoandikwa View Source baada ya kuyapata jaribu ku-click (Ingia) ktk hayo maandishi basi baada ya hapo utajua code zilizotengeneza hiyo website au blog pia utajua mambo mengi zaidi ukiziona hizo code.

Sasa basi kutokana ya kwamba internet ni chombo kizuri na kibaya pia nimeweza kuwaletea dawa itakayo ondoa hilo tatizo. Dawa yenyewe itaenda kutibu pale palipo na tatizo ambapo ni kuweza kuzima uwezo wa mtu yoyote kuweza ku-right click akiwa ndani ya blog au website yako!!

Yafuatayo ni maelekezo ya kuweza kuzima right click mouse:

1: Sign In ktk Blog yako

2: Ukifika ktk Dashboard, Click "Change Settings" alafu Click sehemu ya "Template".

3: Ukishafika kwenye Template tafuta wapi yalipo haya maandishi: <body>

4: Baada ya kuyapata hayo maandishi chini yake weka haya maandishi:

Kutokana na ya kwamba blog inakataa kuonesha hizi code naomba bonyeza hapa kuweza kuzipata hizi code.

5: Baada ya kuzipata hizo code fanya kama nilivyo elekeza hapo juu (3 - 4) alafu mwisho wake naomba click save template changes alafu click republish your blog.
Kuanzia sasa utakuwa umeweza kuzuia watu wasione viungo vinavyotengeneza blog au website yako!!!

Kuanzia leo ukitaka ku-copy kitu chochote kwanza chagua cha kuweza ku-copy (select, highlight) alafu unabonyeza ctrl+c au ukitaka ku-paste kitu chochote utabonyeza ctrl+v. Ninapo andika ctrl+v au ctrl+c nina maanisha kwanza bonyeza ctrl ukifuatia na v au c kwa wakati mmoja yaaani usiachie kile ulicho bonyeza mwanzo ukiwa unabonyeza cha pili. Naomba angalia keyboard yako.

mwisho, kumbuka hii inazuia website au blog yako tu hivyo basi utakuwa na uwezo wa ku-right click ktk website nyingine au blog nyingine.

Ukitaka kuweza kuweka ulinzi mzuri ktk computer yako kumbuka kununua software zitakazo linda computer yako, unaweza ku-download vitu vifuatavyo ambavyo ni bure (Download zote mbili):

1: Malicious Software Removal Tool

2: Windows Defender (Beta 2)

3: Kwa ulinzi zaidi baada ya ku-download hivyo vitu hapo juu, wale wanaotumia window xp mnaweza kuimalisha ulinzi kwa kubonyeza Start --> Control Panel --> Security Center--> Na uweze kuona kama Firewall ipo ON, Microsoft Automatic updates ipo ON, Virus Protection ipo ON. Kama hivyo vitu vipo OFF unaweza kuviweka ON na ktk Firewall weka ON alafu chagua don't allow exceptions na mwisho click OK. Kwa ujumla ukifika ktk Security Center utapata maelezo zaidi ya kufanya. Pia kama unatumia window xp service pack1 nakushauri nenda microsoft. na uweza ku-download window xp service pack2 kwasababu sp2 ni imara zaidi kwa ulinzi wa computer yako kuliko sp1.

Software nyingine ambazo ni bure zitakazo weza kulinda computer yako ni (Chagua moja kati ya hizi):

A: Lavasoft Ad-Aware SE

B: Spybot Search & Destroy (S&D)

Kama una pesa ya kununua software mimi naunga mkono (napendekeza) hii bonyeza hapa kusoma zaidi maana hii ni imara sana.

Kumbuka ya kwamba kama ukiwa na software moja usichanganye na nyingine maana zitakuwa zinaingiliana kulinda computer yako na kuweza kufanya hackers kuiba siri zako zilizopo ktk computer yako. Pia kumbuka usi-download kitu chochote usicho kijua ata kama ni kizuri kiasi gani soma kwanza maelezo yote na ndio download au usifungue e-mail yoyote kama hamjui mtu aliye ituma.

Pia unaweza kubonyeza tools hapo juu-->Internet Options-->Security: Internet-->Medium, Local Intranet--> Medium, Trusted Sites--> Medium, Restricted Sites--> High kila unapokuwa ukibadilisha click apply.
Ukiwa hapo hapo ktk Internet Options--> Privacy: Medium High alafu chagua block popups maana popups nyingi ni mwanzo wa spyware na virus wengine. Kama ukitaka kuruhusu popups ambazo unaziamini siku zote bonyeza Ctrl na wakati huo huo click ktk sehemu husika.

Unaweza kujifunza zaidi kwa kuangalia video zifuatazo bonyeza hapa pia angalia hii video.

Kwa habari zaidi kuhusu software mbali mbali bonyeza hapa au unaweza kutembelea microsoft.

Ukiwa na maswali zaidi kuhusu hii nakala naomba niandikie na nitakujibu asap.


Nashukuru.


2 comments:

Anonymous said...

Ahsante kwa utaalamu huu. Kumbe nilikuwa nimelala mlango wazi

Anonymous said...

kaka somo limeenda shule kweli.endelea kumwaga somo