
HISTORIA YA AIRBUS A380 NDANI YA UK
Ndege ya abiria aina ya Airbus A380 yenye viti vya abiria 555 ambayo ni kubwa kuliko zote ulimwenguni imeweza kuingia ktk historia ya kuwa ni ndege ya kwanza ya aina hiyo kutua ktk ardhi ya Uingereza ktk uwanja wa ndege wa Heathrow hii leo 18/05/2006 saa 13:20 mida ya Uingereza ikitokea Berlin, Germany.
Maandalizi ya kuwezesha ndege hiyo kutua ktk uwanja wa Heathrow imewagarimu waingereza ( British Airports Authority) jumla ya 450 Million pounds na pia imetua ktk sehemu impya ( Inayo julikana kama pier 6 ktkTerminal 3) iliyo jengwa na kugarimu jumla ya 105 Million pounds.
Airbus A380 itakuwa ni mshindani mkubwa wa ndege za Boeing, na kuonesha Boeing wapo ktk ushindani nao wametengeneza ndege aina ya 787 Dreamliner kuweza kushindana ambayo inategemewa kuingia ktk soko ifikapo mwaka 2008 na kuweza kubeba abiria kati ya 200 mpaka 350.
Jumla ya gharama zilizo wezesha kutengeneza ndege ya Airbus A380 ni 6 Billion pounds ambapo mpaka sasa kampuni ya Airbus S.A.S imepokea order karibia 159 kutoka kwa mashirika 16 ya ndege zinazotaka kununua aina hii ya ndege.
Bonyeza hapa kusoma orodha ya makampuni na idadi ya ndege walizo order.
Bonyeza hapa kuona video mbali mbali za Airbus A380 pia kama ukitaka kuangalia video nyinginezo zinapatikana kwa kubonyeza hapa.
Mwisho, ingawa hii ni kama historia lakini imeleta mitazamo tofauti ambapo kuna makundi mawili, yanayo kubaliana na technology hii na wanao ipinga kutokana na sababu za mazingira.