Wednesday, May 03, 2006

MAMBO MAPYA
Je ulishawahi kuwa na website au Blog na baadae ukaamua kutengeneza website au blog nyingine kutokana na sababu mbali mbali?

Kama jibu ni ndio ni wazi kwamba baadae uliweza kuwataharifu ndugu, jamaa na marafiki kama umebadilisha anuani ya website au blog ile ya zamani na kuamua kuwapa anuani mpya ili waweze kukutembelea ktk makazi mapya.

Sasa leo hii nakuja na code zitakazo kukuondolea tatizo la kuambia watu wote kwamba anuani yako ya website imebadilika, cha kufanya hapa ni kufuata malelekezo yafuatayo:
1(a): Sign In ktk Blog ile ya zamani

1(b): Ukifika ktk Dashboard, Click -->Change Settings-->Template

1(c): Ukifika ktk Template tafuta wapi yalipo haya maandishi head yakianza na tags < na kuishia na tag > na baada ya kuyapata hayo maandishi chini yake weka code zifuatazo, bonyeza hapa kuzipata.

2 (a) Utafanya hivyo hivyo ata ktk website yako ambayo ni tofauti na blog, Chakufanya nenda ktk sehemu zilipo code zinazo tengeneza website yako na tafuta maandishi head yakianza na tag < na kuishia na tag > ambayo yapo mwanzo mwanzo mwa code zilipo anzwa kuandikwa na uweke hizi code.

Kuna code za aina mbili ambazo kazi zake zote ni za aina moja sasa mtachagua ni code zipi mtazitumia ktk ya hizo mbili (Yaani chagua moja tu).
Ukikuta sehemu nimeandika "weka anuani mpya hapa" unabidi muweke anuani zenu za website au blog mpya mfano http://vijimamboz.blogspot.com hii ni kama ingekuwa mimi.

3: Mwisho, click save template changes alafu click republish your blog au wenye website tofauti na blog click Save changes.

Basi baada ya kumaliza hapo tu watu wakiwa wanaenda ktk ile website au blog ya zamani watapelekwa moja kwa moja katika makazi mapya ( Yaani ktk website au blog yako mpya).

Ukiwa na maswali zaidi kuhusu hii nakala naomba niandikie na nitakujibu asap.

Nashukuru.

No comments: